@liputan6com: Tentara Nasional Indonesia Angkatan Darat (TNI AD) menyiapan ribuan hektare lahan untuk memperkuat pasokan bahan pangan bagi Satuan-Satuan Pelayanan Pemenuhan Gizi (SPPG) di berbagai wilayah di Indonesia. #kasadmaruli #mbg #pasokanbahanpangan #lip6an #Caroumusik

liputan6.com
liputan6.com
Open In TikTok:
Region: ID
Sunday 02 November 2025 05:00:18 GMT
9063
60
2
7

Music

Download

Comments

dim90568
Dim :
pertama min
2025-11-02 05:04:04
0
silverquin371
sinaloa :
makin lama makin koplak
2025-11-02 11:15:20
0
widhieantara
Va Widhie :
kok kayak yg sebelah
2025-11-02 08:53:46
0
To see more videos from user @liputan6com, please go to the Tikwm homepage.

Other Videos

Binti yangu alikasirikiana na mume wake, akarudi nyumbani kwangu na mtoto wake mdogo wa kike. Kila mara alipokuwa akiondoka kwa mumewe, nakurudi nyumbani nilikuwa namwambia:
Binti yangu alikasirikiana na mume wake, akarudi nyumbani kwangu na mtoto wake mdogo wa kike. Kila mara alipokuwa akiondoka kwa mumewe, nakurudi nyumbani nilikuwa namwambia: "Haiwezekani uache nyumba yako," kisha namrudisha. Lakini safari hii hakutaka kurudi kabisa. Aliponiambia kilichotokea, nilielewa kuwa kosa lilikuwa la mkwe wangu. Nikamuambia: "Sawa mwanangu, bado ni mume wako na baba wa mtoto wako, nitakurudisha mwenyewe kwake," Hata ingawa hakuwahi hata kupiga simu kuulizia angalau hali ya mtoto wake. Nikambeba binti yangu na tukaenda kwa mume wake. Tulipofika Yeye akatangulia mbele akagonga mlango nikiwa mimi nimebaki nyuma. Mume wake alipofungua mlango, moja kwa moja akamwambia: "Kama wazazi wako wanaweza kukulisha, kwanini wakurudishe kwangu?" Pale pale niliganda sakafuni, maneno yake yakanichoma kama moto. Akanigeukia kwa mshangao, akaniambia kwa aibu: "Karibu, baba mkwe." Nikajibu: "Wallahi tunaweza kumlisha, lakini inaonekana wewe hufai kuwa na mke. Sasa hivi niko naye na ninamlisha yeye na mtoto wake. Lakini siku pesa zikiisha, nitakurudishia tena. Nikamchukua binti yangu tukaondoka, machozi yakitiririka usoni mwangu kwa huzuni. Kwa sababu heshima na jitihada zetu za kuokoa ndoa ya binti yetu aliziona kama udhaifu na kutoweza. Nilimwambia binti yangu: "Nitakata sehemu ya mwili wangu nikulishe wewe na mtoto wako. Usihofu kitu chochote." Binti yangu akasema: "Wallahi, baba, kila mara alikuwa akinitukana kwa sababu ya umasikini wetu, na ingawa aliponioa hakuwa na chochote, baada ya kupata neema ya Mungu alianza kuniudhi kila siku… Lakini sikuwahi kuwaambia ili msiumie." Mimi naingiatu chumbani kwangu nikiwa nimevunjika moyo, nikaanza kujiuliza kama nilifanya kosa kumrudisha mwanangu nyumbani na kuharibu ndoa ya mwanangu. Nikaanza kumuomba Mungu amliwaze binti yangu na amchagulie lililo jema. Siku zikapita, nikahisi kuwa Mungu ananibariki na kunipa riziki. Mkwe wangu akanipigia simu, akaniuliza: "Binti yako anarudi lini nyumbani kwake?" Kila mara nikamjibu: "Bado naweza kumlisha yeye na binti yako." Akaanza kunitishia kuwa atampa talaka. Nikamwambia: "Hiyo siyo hasara." Subhanallah, nikahisi nguvu. Nilihisi kuwa Mungu atamtendea haki binti yangu. Siku moja akamtumia binti yangu barua ya talaka… Binti yangu aliumia sana kwa ajili ya mtoto wake. Nikamuambia: "Mola wako atakuchagulia kilicho bora." Siku zikaenda, na Mungu akaendelea kunipa riziki. Kwa sababu binti yangu alikuwa akiomba dua kila wakati: "Mungu akupe kwa ajili ya mema uliyotutendea." Nikaanza kuamini kuwa uwepo wa binti yangu ni baraka katika nyumba yangu. Na kuwa Mungu ananipa riziki kwa sababu yake, hasa baada ya hali ya aliyekuwa mumewe kudorora baada ya talaka. Baada ya mwaka mmoja, kijana mwenye maadili na familia nzuri alimposa binti yangu. Alikubali kulea mtoto wake pia. Nilifurahi sana kwa sababu Mungu alijibu dua zangu. Binti yangu akaolewa, miaka ikapita… Siku moja akarudi nyumbani akiwa amegombana na mume wake mpya. Aliponiambia kilichotokea, nilielewa kuwa safari hii kosa lilikuwa la binti yangu. Nikamuambia: "Twende nikurudishe kwa mumeo." Nikamsindikiza huku moyo wangu ukidunda… Niliogopa kusikia maneno kama yale ya zamani. Nikamuambia binti yangu: "Nitangulie ukagonge mlango." Binti yangu akaniangalia na kusema: "Sawa baba, nitaenda peke yangu." Lakini nikasisitiza msimamo wangu. Akapiga hodi, mumewe alipofungua mlango akamwambia: "Unajua nyumba hii si nzuri bila wewe." Kisha akaniangalia na kusema: "Baba mkwe, wewe mwenyewe umemleta... Wallahi umenitukuza sana." Pale pale nikaanza kulia, machozi yakitiririka kama mto. Mkwe wangu akastaajabu, akaniuliza: "Baba mkwe kuna nini?" Nikajibu kwa sauti ya kubanwa na maumivu ya furaha: "Sasa nimepata amani kuhusu binti yangu. Naweza kufa nikiwa na furaha. Mungu akupe malipo mema kama ulivyonifariji." Mafunzo Kutoka Kisa Hiki Cha Kweli: 1.Upendo wa mzazi kwa mtoto hauna kikomo: Baba huyu alijitoa kwa moyo wote kuhakikisha binti yake anapata heshima, hifadhi na furaha. Alivumilia kudhalilishwa, akahisi maumivu kwa ajili ya mwanawe, lakini hakumuacha. #ukumbushokwetusote

About